Sunday, April 22, 2012

Taswira Za Ziara Ya Rais Wa Zanzibar Dk Ali Shein Huko Kusini Pemba



Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,Dk.Ali Mohamed Shein,akifungua pazia kuashiria ufunguzi wa Tangi la Maji la Ziwani Wilaya ya Chake chake Pemba, akiwa katika ziara ya kutembelea miradi mbali mbali ya kijamii ya Mkoa wa Kusini Pemba jana
Rais wa zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein,akisalimiana na Viongozi wa Vikosi vya Ulinzi ambao ni Wajumbe wa Kikosi cha (Task Force), ya Taifa kuhusu uvunaji wa zao la karafuu,alipowasili katika viwanja vya ukumbi wa Kiwanda cha Makonyo Wawi Pemba akiwa katika ziara ya Mkoa wa Kusini Pemba jana
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,Dk.Ali Mohamed Shein,akisalimiana na Viongozi wa mamlaka ya Maji,alipowasili Ziwani katika ufunfuzi wa tangi la Maji katika shehia hiyo,akiwa katika ziara ya kutembelea miradi mbali mbali  ya kijamii ya Mkoa wa Kusini Pemba jana
Naibu Waziri wa Biashara,Viwanda na Masoko Thuwaiba Edington Kisasi,akimkabidhi zawadi Rais wa zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein,ya tunzo ya karafuu ya mwaka 2011-2012,katika mkutano wa ufungaji wa msimu wa zao la Karafuu,hafla hiyo ilifanyika katika ukumbi wa mikutano wa Kiwanda cha Makonyo Wawi Pemba
Rais wa zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein,akizungumza na Kikosi kazi cha (Task Force) ya Taifa kilichoshuhulikia uvunaji na uuzwaji wa zao la karafuu,katika ukumbi wa  Kiwanda cha Makonyo Wawi Pemba,Rais aliufunga Msimu wa zao hilo kwa mwaka 2011-2012 jana,akiwa katika ziara ya Mkoa wa Kusini Pemba
Rais wa zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein,akiwa katika picha ya pamoja na Kikosi kazi (TaskForce) ya taifa kuhusu uvunaji wa zao la karafuu huko kiwanda cha Makonyo Wawi ,Wilaya ya Chakechake Pemba , akiwa katika ziara ya Mkoa wa Kusini Pemba jana.Picha na Ramadhan Othman,Ikulu-Zanzibar

No comments:

Post a Comment