Tuesday, May 29, 2012

Mustafa Sabodo Atoa Billioni 5 Kwa Ajili ya Ujenzi wa Jengo la Kuegesha Magari Jijini


 Meya wa Manispaa ya Ilala, Jerry Silaa akimkabidhi Mfanyabiashara maarufu nchini, Mustafa Sabodo vibali vya ujenzi wa jengo hilo, kushoto ni  Mwenyekiti wa Madhehebu  ya Khoja Shia Shiraz Walji
--
MFANYABIASHARA maarufu nchini, Mustafa Sabodo ametoa zaidi ya sh.bilioni 5 kwa madhehebu ya Khoja Shia Ithnaashri Jamat kwa ajili ya kujenga jengo la maegesho ya magari.
 
Akizungumza katika hafla ya kupokea vibali vya ujenzi wa jengo hilo Dar es Salaam leo kutoka kwa Meya wa Manispaa ya Ilala, Jerry Silaa alisema jengo hilo litasimamiwa na madhehebu hayo.
 
Alisema jengo hilo lililopo katika mitaa ya India na Morogoro la ghorofa 14 litakuwa na uwezo wa kuhifadhi magari 180 kwa wakati mmoja.
 
Silaa alisema fedha zitakazopatikana kwa malipo ya maegesho ya magari katika kipindi cha miaka 10 zitafanya kazi ya kuchimba visima katika maeneo mbalimbali ya nchi yetu.Meya alisema kwa muda mrefu Jiji la Dar es Salaam limekuwa likikabiliwa na maeneo ya kuegesha magari na kuwa jengo hilo la kwanza kubwa litakuwa ni mkombozi mkubwa.
 
"Kwa muda mrefu tumekuwa na matatizo ya kuegesha magari katika jiji letu hivyo msaada aliotoa ndugu yetu Sabodo kwa madhehebu hayo ya ujenzi wa maegesho hayo itasaidia sana kupunguza tatizo hilo," alisema Silaa.
 
Alisema Manispaa imepokea jambo hilo kwa mikono miwili na ndio maana imekamilisha vibali ili ujenzi huo uende pasipo kikwazo chochote.
 
Alisema jengo hilo litaitwa Sabodo Car Park jambo litakalo weka kumbukumbu ya mchango wake katika kufanikisha shughuliza za maendeleo.
 
Mwenyekiti wa Madhehebu hayo Shiraz Walji, alimshukuru Sabodo kwa msaada wake huo na kuahidi kusimamia vizuri mradi huo ambao utakuwa wa manufaa kwa Watanzania wote.

Msanii wa filamu Elizabeth Michael (Lulu) Atinga Mahakama Kuu



Msanii wa filamu Elizabeth Michael (Lulu) akiwa amezungukwa na walinzi kwenye Mahakama Kuu Dar es Salaam jana kutokana na tuhuma zinazomkabili za kuhusishwa na kifo cha msanii mwenzake Steven Kanumba.Na Mpigapicha Wetu

TASWIRA ZA SIMBA SC WALIVYOSHEREHEA UBINGWA WAO DAR LIVE



 Baadhi ya wachezaji wa Simba SC wakishangilia pamoja na kombe lao wakati wakipita katika mitaa ya jiji la Dar es Salaam jana.
 Mashabiki na wapenzi wa Simba SC wakiwa katika  msafara kuelekea katika Ukumbi wa Dar Live kusherehekea ubingwa wa timu yao jana.
Wachezaji na viongozi wa Simba wakifungua shampeini wakati wakisherehekea ubingwa wao ndani ya ukumbi wa Dar Live jana.
 Naibu Waziri Amos Makala akimvisha medali Uhuru Selemani.
 Meneja wa Global Publishers Ltd, Abdallah Mrisho (kulia) akimkabidhi nahodha wa Simba SC, Juma Kaseja shilingi milioni 3 zilizotolewa na Dar Live kama pongezi kwa timu hiyo kwa kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom 2011/2012.
Wachezaji wa Simba wakipata menyu pembeni ya kombe lao.
 Baadhi ya mashabiki waliohudhuria sherehe hizo.
 Wachezaji na viongozi wa timu ya Simba wakiwa na Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Amos Makalla (katikati aliyeshika kombe).
Mashabiki wa Simba wakiingia ndani ya Ukumbi wa Dar Live tayari kwa sherehe za ubingwa.
---
TIMU ya Simba SC ya jijini Dar jana ilisherehekea ubingwa wake wa 2011/2012 pamoja na mashabiki wake katika ukumbi wa burudani wa DAR LIVE. Sherehe hizo zilitanguliwa na msafara wa magari, pikipiki na watembea kwa miguu ambao walianzia safari yao makao makuu ya klabu hiyo Mtaa wa Msimbazi  na kupitia mitaa kadhaa ya jiji kabla ya kumalizikia katika ukumbi wa Dar Live. Katika msafara huo wachezaji wa Simba walikuwa katika lori la wazi lililopambwa bendera na vitambaa vya rangi nyekundu na nyeupe huku wakiwa na kombe lao walilolibeba

Kama Kawaida Daily Mail Latoa Taswira Za Majangili Jinsi Wanavyokatili Wanyama Mbuga ya Mikumi

 Weak: The animal was so sick it struggled to raise its head as park wardens approached
 Lucrative: Many of the snares are set by poachers who then butcher the animals for their parts which are used in traditional Chinese medicine
 Desperately injured: The young male lion cub was spotted in Mikumi National Park in Tanzania with a poacher's snare twisted cruelly round his neck
 Doomed to die: The wire was twisted so tight that the lion was unable to eat
The final journey: The lion slopes off into the long grass of the park where he would soon die either of starvation or infection
--
Wire snare caught so tightly around his neck he cannot eat, this young male lion is doomed to die a slow and agonising death.Within a matter of days he will be lying in the African bush gasping his last breath.

Nor is he alone in his grim fate. The sight is increasingly common in parts of the continent when a growing number of lions have fallen victim to poaching.Kwa Habari zaid

Jumuiya ya Maimamu Zanzibar (JUMAZA):'' Tunaomba Waislamu Wote Kurudi Majumbani na Kuendelea na Shughuli Zao za Kawaida za Maisha na Wasijihusishe na Kitendo Chochote Cha Uvunjifu wa Amani Maimamu wote Tunaomba Wawatake Waumuni Wao Kutunza Amani Kama Mafundisho ya Dini Yetu Yanavyotuelekeza ''.

Katibu Mtendaji wa Jumuiya ya Maimamu Zanzibar (JUMAZA) Muhiddin Zubeir Muhiddin


Watukufu waislam,
Assalamu Alykum Warahmatullah Wabarakatu.
Kwanza kabisa tunataunguliza shukurani kwa Allah (S.W) kwa uwezo wake kutuwezesha kuishi katika visiwa hivi kwa salama na amani licha ya kupita katika mikiki mbali mbali. Aidha sala na salamu zimfikie Mtume Muhammad (S.A.W), Mtume ambaye ametufundisha dini ya amani inayotutaka kuishi kwa amani, mapenzi na umoja katika jamii.
 
Watukufu Waislam,
Kufuatia kukamatwa kwa Sheikh Mussa Juma ambaye ni muhadhiri wa dini ya kiislam hapo jana tarehe 26/05/2012 kumejitokeza vitendo vya uvunjifu wa amani vinavyodaiwa kufanywa na watu wanaotaka kuachiwa kwa sheikh huyo sambamba na matumizi ya nguvu ya jeshi la polisi kukabiliana na watu hao, hali ambayo imesababisha kuvunjika kwa amani, watu kuishi kwa taharuki, khofu kutawala katika jamii, kusita kwa shughuli za maisha kwa wakazi wa Manispaa ya Mjini Unguja pamoja na kusababisha matatizo ya usafiri katika manispaa hiyo.

Katika muktadha huu Jumuiya ya Maimamu Zanzibar (JUMAZA) inawataka waislamu wote kurudi majumbani na kuendelea na shughuli zao za kawaida za maisha na wasijihusishe na kitendo chochote cha uvunjifu wa amani. Maimamu wote tunaomba wawatake waumuni wao kutunza amani kama mafundisho ya dini yetu yanavyotuelekeza. Sambamba na hili maimamu waendelee kuiombea dua nchi kudumu katika usalama na amani.

JUMAZA inawataka waumuni wote wafahamu kuwa kuhusu watu waliokamatwa na kuzuiliwa na jeshi la polisi mpaka sasa, viongozi wa taasisi wa Jumuiya za kiislamu wanafanya kila juhudi kuzungumza na viongozi wa kitaifa na jeshi la polisi katika kulitafutia ufumbuzi suala lililojitokeza na hatua yoyote itakayofikiwa waislamu watajuilishwa.

Wabilahi Tawfiq
Imeandaliwa na;
Muhidin Zubeir Muhidin
Katibu Mtendaji wa JUMAZA

MBUNGE WA MBEYA MJINI(CHADEMA)JOSEPH MBILINYI ‘SUGU’ KUTOA BURUDANI KALI DAR LIVE JUMAPILI HII

Mr II akiongea na waandishi wa habari juu ya onyesho hilo.

Mr II akisisitiza jambo kwa  waandishi wa habari juu ya onyesho hilo.
 Mratibu wa Burudani na Matukio Dar Live, Juma Mbizo (kushoto) akiwa na Mr II.

Meneja Mkuu wa Global Publishers Abdalah Mrisho (kushoto) akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu burudani itakayotolewa na Sugu akiwa na wasanii wengine wakali   ambao ni pamoja na Professor J na Juma Nature.  Kulia ni Mratibu wa Shoo za Wasanii Dar Live, Luqman Maloto.

  Baadhi ya waandishi wa habari wakimsikiliza mkali huyo.

Check:Taswira Zaidi Ya Jinsi Mambo Yalivyokua Huko Zanzibar


Saturday, May 26, 2012

Mkutano wa Kujadili Maendeleo ya Matumizi ya Nishati Karne ya 21 Kwa Nchi za Afrika Wamalizika Nchini Afrika Kusini


 Pichani shoto ni Rais Mtsaafu wa Zanzibar,Mh Abeid Aman Karume akifafanua jambo mbele ya wageni waalikwa mbalimbali waliofika kwenye mkutano huo uliohusu maendeleo ya matumizi ya nishati karne ya 21 kwa nchi za Afrika
 Balozi Charles Stith  ambaye aliwahi kuwa balozi wa Marekani nchini Tanzania (Mratibu mkuu wa mkutano),akifafanua jambo kwa wageni waalikwa.
  Pichani juu ni wageni waalikwa mbalimbali waliofika kuhudhuri mkutano huo wa maendeleo ya matumizi ya nishati karne ya 21 kwa nchi za Afrika
  Mmoja wa wageni waalikwa akichangia jambo.
  Wageni waalikwa wakifuatilia jambo wakati mkutano ukiwa unaendelea. 
 Wageni waalikwa mbalimbali wakihudhuria mkutano wa kujadili  maendeleo ya matumizi ya nishati karne ya 21 kwa nchi za Afrika,Mkutano huo uliowakutanisha Marais Wastaafu nane wa Afrika,umefikia tamati jana ndani ya chuo kikuu cha Witwatersrand, jijini Johannesburg, Afrika Kusini .
 Pichani shoto ni Rais Mtsaafu wa awamu ya pili wa Tanzania,Mh Ally Hassan Mwinyi akiagana na Balozi Charles Stith  ambaye aliwahi kuwa balozi wa Marekani nchini Tanzania (Mratibu mkuu wa mkutano), mapema jana jioni,mara baada ya mkutano wa siku tatu uliohusu kujadili  maendeleo ya matumizi ya nishati karne ya 21 kwa nchi za Afrika,Mkutano huo uliowakutanisha Marais Wastaafu nane wa Afrika,umefikia tamati jana ndani ya chuo kikuu cha Witwatersrand, jijini Johannesburg, Afrika Kusini .
Pichani shoto ni Rais Mtsaafu wa awamu ya tatu wa Tanzania,Mh Benjamin Mkapa akiagana na Balozi Charles Stith  ambaye aliwahi kuwa balozi wa Marekani nchini Tanzania mapema jana jioni,mara baada ya mkutano wa siku tatu uliohusu kujadili  maendeleo ya matumizi ya nishati karne ya 21 kwa nchi za Afrika,Mkutano huo uliowakutanisha Marais Wastaafu nane wa Afrika,umefikia tamati jana ndani ya chuo kikuu cha Witwatersrand, jijini Johannesburg, Afrika Kusini .
 Pichani shoto ni Rais Mtsaafu wa Zanzibar,Mh Abeid Aman Karume akiagana na Balozi Charles Stith  ambaye aliwahi kuwa balozi wa Marekani nchini Tanzania (Mratibu mkuu wa mkutano), mapema jana jioni,mara baada ya mkutano wa siku tatu uliohusu kujadili  maendeleo ya matumizi ya nishati karne ya 21 kwa nchi za Afrika,Mkutano huo uliowakutanisha Marais Wastaafu nane wa Afrika,umefikia tamati jana ndani ya chuo kikuu cha Witwatersrand, jijini Johannesburg, Afrika Kusini
Wahariri wa vyombo vya habari kutoka nchini Tanzania,wakiagana na Marais Wastaafu wa Tanzania,mara baada ya mkutano wa kujadili  maendeleo ya matumizi ya nishati karne ya 21 kwa nchi za Afrika,Mkutano huo uliowakutanisha Marais Wastaafu nane wa Afrika,umefikia tamati jana ndani ya chuo kikuu cha Witwatersrand, jijini Johannesburg, Afrika Kusini .
Pichani shoto ni Rais Mtsaafu  NicĂ©phore DieudonnĂ© Soglo wa Benin akiagana na Balozi Charles Stith  ambaye aliwahi kuwa balozi wa Marekani nchini Tanzania (Mratibu mkuu wa mkutano), mapema jana jioni,mara baada ya mkutano wa siku tatu uliohusu kujadili  maendeleo ya matumizi ya nishati karne ya 21 kwa nchi za Afrika,Mkutano huo uliowakutanisha Marais Wastaafu nane wa Afrika,umefikia tamati jana ndani ya chuo kikuu cha Witwatersrand, jijini Johannesburg, Afrika Kusini
 Kushoto ni Balozi Charles Stith  ambaye aliwahi kuwa balozi wa Marekani nchini Tanzania (Mratibu mkuu wa mkutano),Rais Mtsaafu wa awamu ya pili wa Tanzania,Mh Ally Hassan Mwinyi pamoja na  Rais Mstaafu wa Zanzibar,Mh Abeid Aman Karume wakiwa katika picha ya pamoja jioni ya jana na Wahariri wa vyombo vya habari kutoka Tanzanania,mara baada kumalizika kwa mkutano wa kujadili  maendeleo ya matumizi ya nishati karne ya 21 kwa nchi za Afrika,Mkutano huo uliowakutanisha Marais Wastaafu nane wa Afrika,umefikia tamati jana ndani ya chuo kikuu cha Witwatersrand, jijini Johannesburg, Afrika Kusini .
 Baadhi ya Wanafunzi kutoka chuo kikuu cha Dar Es Salaam (UDSM) wakiwa katika picha ya pamoja mapema leo mara baada ya kushiriki mkutano wa kujadili  maendeleo ya matumizi ya nishati karne ya 21 kwa nchi za Afrika,Mkutano huo uliowakutanisha Marais Wastaafu nane wa Afrika,umefikia tamati jana ndani ya chuo kikuu cha Witwatersrand, jijini Johannesburg, Afrika Kusini .Picha na Ahmed Michuzi-Johanneburg

Wabunge Wa Chadema Peter Msigwa na Joshua Nassari Nao Watua Washington DC


 Safari na muziki wameruka na wametua kwa salama na amani, wabunge wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wa kwanza kulia, Nassari Joshua, Dogo Janja akiwa na  Mhe.   Peter Msigwa ndani ya Washington DC
Wanachama wa Chadema Washington DC Anko Ludigo akiwa na Mhe Dogo Janja, Mkereketwa Libe aka Mwangombe, pamoja na Mhe. Peter Msigwa, wakiwa wameshikilia kadi za Chadema ambazo zipo tayari kwa kila  mwenye kupenda mabadiliko ya Tanzania.Picha na Picha na Libe Mwangombe
--
Ndani ya jiji la Washington Dc Wabunge  Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)   waibuka jijini hapa kwa vishindo, huku Watanzania mbali mbali waishio nchini Marekani wakiwasuburi kwahamu siku hiyo ya Jumapili Mei 27, 2012,

Madhumuni ya mkutano huo ni kukutana na Watanzania wanaoishi Nchini Marekani kuzungumza juu ya mpango mzima  wa maendeleo  ya nchi yetu kwa jumla, mkutano huo utahudhuriwa na Mhe. Leticia  Nyerere, Mhe. Zitto Kabwe, Mhe. Nassari Joshua Marufu Dogo Janja na Mhe. Mchungaji Msigw

Friday, May 18, 2012

Takwimu ya fainali ya Ulaya


Bayern na Real Madrid
Klabu ya Bayern imeshinda mechi zake saba za nyumbani mfululizo kuelekea fainali hii dhidi ya Chelsea.
Mara ya mwisho kwa pande hizi mbili kukutana, ilikua katika robo fainali ya mwaka 2005 ambapo Chelsea ilishinda 6-5 kwa jumla ya mabao ya ugenini na nyumbani.
Chelsea na kombe la FA
Wakati huo Petr Cech, John Terry, Ashley Cole, Frank Lampard na Didier Drogba wote walishiriki.
Bayern inataraji kujiunga na Liverpool kama mojapo ya vilabu vitatu vilivyofanikiwa katika mashindano ya Kombe la Ulaya ikiwa watashinda kwa mara ya tano.
Klabu iliyopata ushindi zaidi ya Bayern ni Real Madrid na AC Milan.
Bayern imeshinda mara moja na kushindwa mara mbili mara tatu ilipochuana na upinzani kutoka kwa vilabu vya England.
Hii ni mara ya sita katika Kombe la Ulaya kwa vilabu vya Ujerumani na England kupambana kwenye fainali -na ni mara moja tu ambapo vilabu kutoka Ligi ya Bundesliga kuibuka na ushindi.
Jupp Heynckes-Bayern
Ushindi wa Bayern utamfanya Jupp Heynckes kua kocha wa 19 kushinda kombe hili mara mbili, kufuatia ushindi wake wa 1998 alipokua akiifunza Real Madrid.
Ikiwa uwanja wa nyumbani Bayern imeshinda mechi 13 kati ya 14 za michuano ya Ulaya, huku Chelsea ikiwa imeshinda mara moja tu ikiwa safarini katika michuano ya msimu huu.
Mara pekee ambapo Chelsea ilifikia fainali ilikua mwaka 2008 mjini Moscow iliposhindwa na Manchester United kupitia mikwaju ya pen

Tuesday, May 15, 2012

Watuhumiwa Wa Vurugu Za Mkutano Wa Chadema Nduli Wafikishwa Mahakamani

Wafuasi wa  Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wakifika Kituo cha Polisi Iringa.
Washtakiwa wa kosa la kujeruhi  Ndugu Meshaki Chonanga, Alex Chonanga, Greyson Chonanga na Musa Mtete  wote kwa pamoja wakitoka Mahakamani leo baada ya kusomewa shitaka la kuwajeruhi  Ndugu Suleiman Komba, Peter Mselu na Oscar Sanga. Washtakiwa walikana kosa hilo na kesi yao kuahirishwa mpaka tarehe 25/05/2012

Washtakiwa wakishuka kwenye Karandinga kuingia rumande baada ya kukosa dhamana kutokana na wajeruhiwa  wawili kati ya wale watatu kuwa katika hali mbaya hospitali ya mkoa wodi namba 5.
Wafuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Manispaa ya Iringa wakitokea Mahakamani kuelekea Kituo cha Polisi Iringa wakienda kutaka kupata maelezo juu ya Mlalamikiwa  Mh. Diwani Idd Chonanga ambaye ndiyo mlalamikiwa wa kwanza kutofikishwa Mahakamani baada ya kukamatwa na Polisi na kuachiwa kwa dhamana.
(Picha zote na Said Ng'amilo-Mdau wa Mjengwa Blog Iringa)
 
HATMA YA MAANDAMANO YA WAFUASI WA CHADEMA

Kaimu Kamanda wa Mkoa akiri kutofikishwa kwa Mh. Diwani Idd Chonanga mahakamani leo kwa kuwa aliachiwa kwa dhamana jana katika kituo cha Polisi na kuahidi Mh. Huyo atafikishwa mahakamani kesho tarehe 16/05/2012. Maelezo hayo alipewa Mheshimiwa Mbunge  wa Iringa Mjini Peter Msigwa (Chadema) baada ya kuonana na Kaimu Kamanda ofisini kwake leo.

Rais mpya wa Ufaransa Hollande aapishwa

Francois Hollande ametawazwa kama rais mpya wa Ufaransa, na kumfanya kuwa rais wa kwanza wa kisosholisti kuapishwa katika miaka kumi na saba.
     RAIS MTEULE WA UFARANSA       












Bwana Hollande alisema kuwa anafahamu vyema changamoto ambazo Ufaransa inakabiliana nazo ikiwemo, madeni na uchumi unaojikokota.

Baadaye hii leo rais Hollande atamteua waziri mkuu na kisha kwenda nchini Ujerumani kwa mazungumzo na Chansella Angela Merkel.
Bwana Hollande angependa kufanya mazungumzo zaidi kuhusu mpango wa Ujerumani wa kutafuta suluhu kwa mgogoro wa kiuchumi unaokumba bara la Ulaya.
Hapo jana thamani ya Euro ilishuka masoko ya hisa nayo yakishuka huku hali ya kisiasa nchini Ugiriki ikiendelea kuwa tete.
Mwenyekiti wa baraza la mawaziri wa fedha wa ulaya, Jean-Claude Juncker, alisisitiza hapo jana kuwa watafanya kila wawezalo kuhakikisha kuwa Ugiriki inasalia katika muungano wa Ulaya.
Bwana Juncker anasubiri kuundwa haraka kwa serikali mpya ya Ugiriki siku tisa baada ya kufanyika uchaguzi mkuu.
Lakini pia alionya kuwa Ugiriki haina budi ila kuendelea na juhudi muhimu zilizoanzishwa kuweza kuokoa uchumi wake licha ya sera hizo kupingwa na wapiga kura wengi.
Wengi mjini Berlin wanamshuku bwana Hollande. Hawapendi kuwa wakati wa kampeini zake alionekana kupinga mipango ya kupunguza matumizi ya serikali kwa lengo la kuokoa uchumi pamoja na kuukuza.
Wengi walitafsiri hilo kama juhudi za Ufaransa kutaka kuongoza tena muungano wa Ulaya.