Monday, May 14, 2012

China: Je ndio nchi inayoongoza kwa werevu duniani?

Watoto wa shule nchini China
Matokeo ya china katika mitihani ya kimataifa shuleni, ambayo haijawahi kuchapishwa, ni ya kuridhisha saana. Hii ni kauli ya Andreas Schleicher, ambaye anahusika na mitihani ya kimataifa ya Pisa.
Mitihani hii hufanywa baada ya kila miaka mitatu na kuandaliwa na shirika la ushirikiano wa kiuchumi na maendeleo. Lengo lake huwa ni kuchunguza uwezo wa mtoto kusoma, kufanya hesabu na sayansi.
Mitihani ya Pisa, imetumika kama kigezo cha kimataifa kwa wanafunzi kote duniani.
Matokeo haya yanaonyesha kuwa China ina mfumo wa elimu ambao unapiku nchi za magharibi.
Licha ya wengi kupiga darubini sana hali ya kiuchumi na kisiasa nchini China, ripoti hii inatoa fursa kwa watu kuona nchi hiyo inavyoelimisha kizazi kijacho.
Wanajizatiti sana.
Mitihani ya Pisa mwaka 2009, ilionyesha wazi kuwa Shanghai ilikuwa juu kwenye orodha ya waliofanya vyema kielimu kimataifa.
Hata hivyo haikuwa wazi ikiwa Shanghai pamoja Hong Kong ambayo pia ilifanya vizuri sana, ziliwakilisha ipasavyo kikanda au kulikuwa na maeneo mengine ambayo yalifanya vizuri zaidi. .
Bwana Schleicher anasema kuwa matokeo ambayo hajachapishwa yanaonyesha kwa wanafunzi katika maeneo mengine ya China pia wanafanya vyema sana.
Andreas Schleicher " Inategemea nafasi wanayopewa wanafunzi kufanikiwa maishani"
"Hata katika maeneo ya vijijini na maeneo yaliyotengwa kiuchumi, ni wazi kuwa wanafunzi wana bidii sana" alisema Schleicher.
Aliongeza kuwa matokeo ya mitihani yanaonyesha wanafunzi wanajizatiti sana kuweza kufanikiwa licha ya mazingira magumu sawa na pengo lililoko kati ya wanafunzi kutoka familia maskini na zile tajiri.
Bwana Schleicher alielezea kushangazwa zaidi na matokeo ya shule za vijijini ikilinganishwa na alichoshuhudia mijini kama vile Shanghai. Yaani hali wanavyojizatiti wanafunzi ni ya kutia moyo.
Nchini China msingi wa maisha bora ni elimu, na kulingana na utafiti huo hilo lilibainika wazi kwani wanafunzi wanaelewa kuwa bila elimu, maisha yako hayatakuwa mazuri.
Matokeo ya wanafunzi wanaotoka famailia zisizojiweza nchini China, bila shaka inaweza kuonewa wivu na nchi za magharibi kulingana na bwana Schleicher.
Katika juhudi zake kupata picha halisi, mitihani ilifanywa katika mikoa tisa ikiwemo katika maeneo yenye viwango vya juu vya umaskini, katika maeneo yenye kipato cha kadri na mwishowe katika maeneo yenye matajiri wengi.
Wanafunzi wa shule ya upili ya Nanjing wanafahamu vyema kauli mbiu yao " lazima niende katika chuo kikuu" walisika wakisema nje ya shule yao.
Hata hivyo serikali ya China imekataa kuruhusu kuchapishwa kwa matokeo ya mitihani hiyo.
Lakini bwana Schleicher anasema kuwa matokeo hayo yanaonyesha picha halisi ya jamii kuekeza kwa ujumla katika elimu.
Wanafunzi nchini China
Katika ziara yake katika mkoa mmoja, bwana Schleicher anasema aliona majengo ya shule yakiwa yanapendeza sana.
Katika nchi za magharibi, ungedhani majengo hayo ni maduka ya kifahari.
Pia kulikuwa na tofauti kubwa kati ya wanafunzi vijana, walioulizwa kwa nini wanadhani wanafunzi wanafaulu sana shuleni.
Raia kutoka Marekani husema ni bahati tu , ni mtu kuzaliwa akiwa ana akili ya kujua mfano hesabu na ikiwa hiyo nidio maoni ya wengi wanafunzi huonelea ni bora kufanya anachoona anaweza mwenyewe.
Barani Ulaya elimu ni juu ya urithi, mfano wanafunzi husema babangu alikuwa seremala kwa hivyo na mimi nitakuwa seremala, haoni haja ya kufanya bidii kusoma.
Nchini China wanafunzi wengi husema inategemea bidii yangu, ikiwa nitafanya bidii bila shaka nitafanikiwa masiahani.

BENKI KUU: HAZINA YA TAIFA IMEKAUKA?

Zitto Kabwe, Mb.

Benki Kuu ya Taifa lolote ndio taasisi pekee yenye takwimu zote nyeti na za uhakika zinazohusu uchumi wa Taifa hilo. Katika tovuti ya Benki Kuu ya Tanzania eneo la Machapisho kuna Taarifa nyeti sana mbili, Mapitio ya Uchumi ya Mwezi (Monthly Economic Review) inayotoka kila Mwezi katika Mwaka na Mapitio ya Uchumi ya Robo Mwaka (Quarterly Economic Bulletin). Taarifa hizi hutoa taarifa kuhusu masuala yote muhimu yanayohusu Uchumi wa Jamhuri ya Muungano na Uchumi wa Zanzibar ikiwemo taarifa za Mfumuko wa Bei, Mapato na Matumizi ya Serikali, Mwenendo wa Biashara ya

Kimataifa na Deni la Taifa.

Ukienda kwenye tovuti ya Benki Kuu leo utakuta Taarifa hizi. Lakini Taarifa hizi zimeishia Desemba mwaka 2011 zikitaarifu masuala ya Uchumi ya Mwezi Novemba na robo ya mwaka inayoishia Desemba. Ukitaka kujua Bajeti ya Serikali na mwenendo wake hutapata taarifa za sasa bali za Mwezi Novemba mwaka 2011, miezi sita nyuma. Huu sio utendaji uliotukuka. Hii ni kuficha taarifa kwa wananchi. Taarifa zinafichwa ili iwe nini? Nani anafaidika na kufichwa kwa taarifa muhimu kama hizi?

Kuna tetesi kwamba Hazina ya Taifa (Hifadhi ya Fedha za kigeni – foreign reserve) inakauka, kwamba tuna hifadhi ya kuagiza bidhaa nje kwa mwezi mmoja tu. Niliposikia tetesi hizi sikuamini. Nilipoenda katika tovuti ya Benki Kuu ili kuweza kuwa na habari rasmi (authoritative) nimekuta takwimu za Novemba 2011.

Takwimu ya Mfumuko wa Bei iliyoko kwenye tovuti ya Benki Kuu ya Tanzania ni ya mwezi Novemba mwaka 2011!

Ukitaka kujua mwenendo wa Bajeti ya Serikali kama makusanyo ya Kodi na Matumizi utapata Taarifa ya Mwezi Novemba mwaka 2011.

Ukitaka kujua manunuzi ya Mafuta (fuel imports) kwa miezi 3 ya mwanzo ya mwaka 2012 ili kuweza kuona namna Umeme wa dharura umeathiri urari wetu wa Biashara ya Nje hupati taarifa hiyo katika tovuti ya Benki Kuu.

Taarifa zinafichwa.

Ndio. Zinafichwa tena makusudi maana taarifa hizi zipo Benki Kuu. Huu ni uzembe maana Nchi inawalipa wafanyakazi wa Benki Kuu mishahara minono ili wafanye kazi hizi. Benki Kuu pia imetoa zabuni kwa Kampuni Binafsi kuchapisha Taarifa hizi. Kama Taarifa hazitoki kwa wakati ni wizi. Wizi ambao haupaswi kufumbiwa macho.

Benki Kuu ya Tanzania ipo miezi Sita nyuma. Aibu kubwa sana.

Wakati Rais wa Jamhuri ya Muungano akihakikishia mataifa duniani kuhusu uwazi Serikalini (#OGP), Taasisi kubwa kama Benki Kuu inaficha Taarifa ambazo ni nyeti kwa wananchi na muhimu kwa wafuatiliaji wa sera za Serikali. Rais wa nchi anaongea Buluu, Gavana wa Benki Kuu anasimamia Kijani!

Inaudhi na kukera sana kwenda kwenye tovuti ya Benki Kuu na kukuta taarifa za miezi Sita iliyopita. Benki Kuu hamstahili kuitwa Benki Kuu, labda benki kuu kuu. Rekebisheni jambo hili haraka sana maana kuficha taarifa kwa Umma ni ufisadi. Haki ya kupata taarifa ni haki ya msingi katika Katiba yetu.  Hatutaki kushtukizwa na kuambiwa Hazina ya Taifa imekauka.

Prof. Ndulu hakikisha Taarifa ya Mapitio ya Uchumi wa kila Mwezi imewekwa kwenye tovuti kwa muda mwafaka. Ifikapo mwisho wa Wiki inayoanzia Jumatatu Mei 14, tovuti ya Benki Kuu iwe na Taarifa za miezi yote (Desemba, Januari, Februari, Machi na Aprili). Taarifa hizi ni muhimu ili nasi tutekeleze majukumu yetu ya Kikatiba kama Wabunge, Mawaziri vivuli na Wananchi wa Tanzania.

Sunday, May 13, 2012

Kamanda mmoja wa LRA akamatwa


Jeshi la Uganda linasema kuwa limemkamata afisa mwandamizi wa kundi la wapiganaji la LRA - kundi ambalo limekuwa likiwauwa na kuwateka nyara watu Afrika mashariki na ya kati, kwa zaidi ya miaka 20.
Mpiganaji wa LRA

Kiongozi wa LRA, Joseph Kony anasakwa na Mahakama ya Uhalifu ya Kimataifa, kwa uhalifu wa vitani.
Washauri wa Marekani wamekuwa wakisaidia majeshi ya nchi za Afrika mashariki na kati katika msako wao wa kumtafuta Kony pamoja na wafuasi wake.
Jeshi la Uganda linasema limemkamata kamanda mwandamizi wa LRA, Caesar Achellam kando ya Mto Mbou katika Jamhuri ya Afrika ya Kati.
Limesema Achellam alikuwa na bunduki tu ya aina ya AK-47 na risasi chache.
Ingawa LRA inasemekana kuwa na wapiganaji mia mbili-tatu tu, hata hivo imeleta maafa nchini Uganda, Sudan Kusini, Congo na Jamhuri ya Afrika ya Kati, kwa kuuwa na kuwatesa watu, pamoja na kuwateka nyara watoto wao na kuchoma moto nyumba zao.

Manchester City bingwa Ligi ya England

Manchester City ikifunga mabao mawili zikiwa zimesalia dakika mbili za nyongeza mpira kumalizika, wamefanikiwa kuunyakua ubingwa wa Ligi Kuu ya Kandanda ya England kwa kuwalaza QPR waliocheza wakiwa 10 kwa mabao 3-2 katika mchezo uliomalioza msimu kwa mtindo wa kusisimua.
Wachezaji wa Manchester City wakishangilia ubingwa
Wachezaji wa Manchester City wakishangilia ubingwa
Pablo Zabaleta alikuwa wa kwanza kuipatia bao la kuongoza Manchester City kabla Joleon Lescott kufanya makosa na kumpatia nafasi Djibril Cisse kuisawazishia QPR.
Joey Barton alitolewa nje kwa kadi nyekundu baada ya kukwaruzana na Carlos Tevez lakini alikuwa Jamie Mackie aliyeipatia bao la pili QPR kipindi cha pili.
Huku Manchester United ikiwa imeshailaza Sunderland, Manchester City walionekana kama wangepoteza nafasi ya kuunyakua ubingwa lakini Edin Dzeko akafanikiwa kufunga bao la kusawazisha kwa kichwa na dakika moja baadae Sergio Aguero akapachika bao la ushindi lililoimaliza kabisa QPR.
Hili ni taji la kwanza la Manchester City tangu waliposhinda kombe la Ubingwa wa Ligi daraja la kwanza wakati huo mwaka 1968.
Manchester United imepoteza taji lake la Ligi Kuu ya England, licha ya kuilaza Sunderland baada ya mahasimu wao wakubwa Manchester City kuilaza Queens Park Rangers.
Bao la kichwa lililowekwa kimiani na Wayne Rooney lilioneka kama lingempatia Sir Alex Ferguson ubingwa wa Ligi Kuu ya Kandanda kwa mara ya 13 kwa kipindi chake cha umeneja kwa miaka 20.
Manchester United walikuwa wanadhani wameshinda ubingwa baada ya Manchester City kuwa nyuma kwa mabao 2-1 na zikiwa zinaelekea dakika za nyongeza kumalizika huku mashabiki wao wakianza sherehe za ubingwa.
Lakini taarifa zilizofika kwa mashabiki wa Manchester United kwamba Manchester City wamepachika mabao mawili ya haraka haraka dakika za mwisho ziliwanyamazisha mashabiki hao na wachezaji wao wakaonekana hawaamini wanachokisikia.
Arsenal imefanikiwa kupata nafasi ya tatu na watacheza Ligi ya Ubingwa wa Ulaya msimu ujao moja kwa moja baada ya kuilaza West Brom mabao 3-2, hasa kutokana na makosa ya mlinda mlango wa West Brom Marton Fulop.
Ushindi huo wa 3-2 ina maana kikosi cha Arsene Wenger kimemaliza msimu wakishika nafasi ya tatu.
Fulop alifanya makosa yaliyoipatia Arsenal bao la kuongoza dakika nne tu tangu mchezo ulipoanza kupitia kwa Yossi Benayoun lakini muda mfupi tu West Brom wakafanikiwa kusawazisha.
Lakini walikuwa Andre Santos na Laurent Koscielny waliopiatia Arsenal mabao ya ushindi kwa Arsenal.
Tottenham baada ya kuilaza Fulham mabao 2-0 imefanikiwa kumaliza ligi wakiwa nafasi ya nne lakini watajipatia nafasi ya kucheza Ligi ya Ubingwa wa Ulaya iwapo tu Chelsea itapoteza mchezo wa fainali ya Ubingwa wa Ulaya.
Emmanuel Adebayor alikuwa wa kwanza kuipatia Tottenham bao la kwanza ambapo Fulham nao walikosa nafasi nzuri ya kufunga kwa mkwaju wa Moussa Dembele kugonga mwamba.
Jermain Defoe aliithibitishia Tottenham ushindi baada ya kupachika bao la pili kutokana na mkwaju wa awali alioufumua Aaron Lennon kuwagonga wachezaji wa Fulham.
Ndoto za kucheza Ubingwa wa Ulaya kwa Newcastle ziliyeyuka baada ya Everton kumaliza msimu kwa mtindo wa aina yake katika uwanja wa Goodison Park. Everton walifanikiwa kupata ushindi wa mabao 3-1.
Steven Pienaar aliufungua mlango wa Newcastle kwa mkwaju wa yadi 20 ambao ulimgonga mlinzi wa Newcastle Mike Williamson na kujaa wavuni.
Nikica Jelavic akaiongezea Everton bao la pili sekunde chache baada ya jitahada zake za awali kupanguliwa na mlinda mlango Tim Krul kabla Johnny Heitinga kuongeza bao la tatu.
Chelsea kwa urahisi iliilaza Blackburn mabao 2-1 baada ya kumiliki mpira kwa muda mrefu katika uwanja wa Stamford Bridge.
Chelsea walipumzisha wachezaji wao wengi nyota wakiwa wanajiandaa kwa fainali ya Ubingwa wa Ulaya wiki ijayo, lakini hata hivyo hawakuonesha kandanda ya kuvutia sana.
John Terry aliufungua mlango wa Blackburn kwa bao la kichwa baada ya kuunganisha mkwaju wa juu uliochongwa na Romelu Lukaku na baada ya dakika tatu Raul Meireles akaifungia Chelsea bao la pili.
Chelsea walikosa nafasi nyingi za kufunga lakini Yakubu alionekana mwiba kwa ngome yao baada ya kuipatia Blackburn bao moja katika shambulio la nadra walilofanya.
Danny Graham akiwa amefunga bao lake la 100 tangu aanze kucheza kandanda alifanikiwa kuipatia Swansea ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Liverpool.
Graham alifumua mkwaju akiwa karibu na lango zikiwa zimesalia dakika nne kabla mpira kumalizika na kupata ushindi wa kumbukumbu.
Swansea walimiliki mchezo kwa muda mrefu kipindi cha kwanza na Gylfi Sigurdsson mara mbili alikosa nafasi za kufunga.
Liverpool walibadilika kipindi cha pili na Andy Carroll mpira wa juu alioupiga uliokolewa na mlinda mlango Michel Vorm.
Norwich walimaliza msimu vizuri sana baada ya kupata ushindi rahisi dhidi ya Aston Villa hali iliyoongeza chagizo kwa meneja Alex McLeish.
Mshambuliaji wa Norwich Grant Holt alikuwa wa kwanza kuipatia timu yake bao la kwanza kwa mkwaju wa adhabu ya moja kwa moja na kuandika bao lake la 17 msimu huu.
Simeon Jackson alitumia makosa ya mlinzi wa Aston Villa Carlos Cuellar na kupachika bao la pili akiwa karibu kabisa na lango.
Villa iliwalazimu wamshukuru sana mlinda mlango wao Shay Given, ambaye alifanya kazi ya ziada kupunguza mabao.
Meneja wa Aston Villa McLeish alikuwa akizomewa na mashabiki wa timu yake muda wote wa mchezo ambapo tangu ameichukua timu hiyo msimu huu mambo hayakumuendea vizuri.
Bolton hatimaye wameshuka daraja na msimu ujao hawatacheza tena Ligi Kuu ya Kandanda ya England baada ya kutoka sare na Stoke katika uwanja wa Britannia.
Iwapo Bolton wangeshinda mechi hiyo - huku QPR wakiwa wamefungwa na Manchester City - wangepona na shoka la kushuka daraja, lakini bao la mkwaju wa penalti uliofungwa na Walters likaizamisha.
Mark Davies alikuwa wa kwanza kuipatia bao Bolton na baadae bao lililofungwa na Kevin Davies likaonekana kabisa kufufa uhai kwa Bolton.
Lakini bao la penalti la Walters bada ya Peter Crouch, kufanyiwa rafu ndani ya boksi likaididimiza Bolton na msimu ujao watacheza ligi ya Championship.
Wigan imefanikiwa kupata ushindi wa saba katika mechi tisa ilizocheza na kuepuka kabisa panga la kuwateremsha daraja dhidi ya Wolverhampton Wanderers ambao tayari wameshateremka daraja. Wingan wameshinda mabao 3-2.

Taswira Za Mkutano Wa CHADEMA Wilayani Same,Wazidi Kuvuna Wanachama Wapya Kutoka CCM na Katibu Mkuu wa Chama Cha TLP Same Ajiunga na Chadema


  James Ole Millya akihutubia
 Katibu Mkuu wa TLP Same, Heriel Msolo(kulia) akirudisha kadi jana Mbele ya Mwenyekiti wa Baraza la Vijana BAVICHA, Ngd Jhon Heche(wa pili kushoto)na Aliekuwa mbunge wa Arusha Mjini(CHADEMA), Godbless Lema(Kushoto)
  Vijana wakigombea ofa ya kadi 10 za Millya
  James Ole Millya akisalimiana na mwanachama wa CCM aliahamia CHADEMA Same jana
  Aliekuwa mbunge wa Arusha Mjini(CHADEMA), Godbless Lema akiwasili Same
  Wananchi wa Same wakigombea foleni ya kupatiwa kadi za CHADEMA jana
-- 
Habari na  Seria Tuma

CHADEMA wanaziara ya kichama Wilayani Same kwa siku nne,kuanzia jana hadi jumatatu chini ya Mwenyekiti wa Baraza la Vijana BAVICHA, Ngd John Heche.

Wana mikutano maeneo tofauti ya Wilaya katika kuimarisha chama hicho.Mkutano wa jana ulifanyikia viwanja vya Kwasakwasa Mjini Same kuanzia saa 9 hadi saa 12 jioni

Viongozi waliohudhuria ni pamoja na aliekuwa mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema, Mwenyekiti Bavicha, John Heche, Mweyekiti CHADEMA Kilimanjaro, Augustino Matemu na kiongozi wa vijana Babati, Wilson Mattaka.

Wengine ni James Ole Millya aliekuwa Mwenyekiti UVCCM Arusha, aliekuwa Mjumbe wa NEC CCM kutoka Arusha, Ndg Ally Bananga na aliekuwa Diwani wa Sombetion (CCM). WOte hawa walihamia CHADEMA mapema mwezi huu

Katika mkutano huo kadi nyingi sana zilitolewa na kuasiniwa na John Heche..tena zikigombewa kununua. Lema litoa ofa ya kadi 10 kwa kina mama na Millya nae akatoa ofa ya kuwalipia vijana kumi..

Aliekuwa Katibu Mkuu wa TLP Same, Ndg Heriel Msolo alirudisha kadi ya TLP na kupewa kadi ya CHADEMA na Mwenyekiti wa BAVICHA, John Heche

Lema aliwataka watanzania kutokubali kugwanywa na wanasiasa kwa misingi ya udini na ukabila au ukanda na kueleza kwamba CHADEMA haipiganii maslahi ya kundi lolote katika hayo. Akasema hata yeye hapiganiimaslahi yake binafsi bali ya watanzania.

John Heche aliwataka watanzania kujitokeza kutoa maoni yao kwa tume ya Katiba na kuelekeza kuwa wakatae au wazifanyie mabadiliko makubwa nafasi za uDC au uRC na nyinginezo za kuteuliwa na mtu mmoja. Akadai pia madaraka ya rais ni makubwa na mamabo mengi yameachwa kwa mtu mmoja. hali inayohitaji marekebisho ili kuwe na uwajibikaji wa pamoja..

Saturday, May 12, 2012

CHECK mbinu za ulinzi zitakazo tumika katika mashindano ya OLIMPIKI


Wizara ya Ulinzi ya Uingereza imethibitisha kuwa chombo kama honi, kitatumiwa kama silaha mjini London wakati wa michezo ya Olimpiki.
Mazoezi ya ulinzi kwenye Mto Thames, London
Kelele za chombo hicho zinaweza kuvuma kwa masafa marefu na kuumiza masikio.
Chombo hicho kimetumiwa sehemu kadha za dunia kutawanya mkusanyiko wa watu; na kinatengenezwa Marekani ambako kimearifiwa kuharibu masikio daima.
Lakini Wizara ya Ulinzi inasema kitatumiwa tu kwenye vipaza sauti kuzuwia misafara kwenye Mto Thames; na ni sehemu ya zana kadha zitazotumiwa kuhakikisha usalama wa Olimpiki.
Chombo hicho kinatumiwa kupambana na maharamia wa Somalia.

HAYA NDUGU ZANGU:NAFASI ZA KAZI HIZO (JOBS)



TUTORIAL ASSISTANT/EXAMINATIONS OFFICER
Qualification: Bachelor degree in Educations or equivalent qualifications
Apply: Secretary, Public
Service Recruitment
Box  63100 ,Dar es Salaam
Details:Daily News April 30, 2012
Deadline:  May   14, 2012

ACCOUNTANCY GRADE I
Qualification: Bachelor degree or Advanced Diploma in Accountancy  or equivalent qualifications
Apply: Secretary, Public
Service Recruitment
Box  63100 ,Dar es Salaam
Details:Daily News April 30, 2012
Deadline:  May   14, 2012

SENIOR INTERNAL AUDITOR
Qualification: Bachelor degree or Advanced Diploma in Accountancy and CPA (T) or - ACCA or equivalent qualifications
Apply: Secretary, Public
Service Recruitment
Box  63100 ,Dar es Salaam
Details:Daily News April 30, 2012
Deadline:  May   14, 2012

SENIOR ADMINISTRATOR OFFICER
Qualification: Bachelor degree or Advanced Diploma in Public Administration,Sociology, Human Resource Management or
equivalent qualifications
Apply: Secretary, Public
Service Recruitment
Box  63100 ,Dar es Salaam
Details:Daily News April 30, 2012
Deadline:  May   14, 2012

SENIOR SYSTEMS ADMINISTRATOR
Qualification: Must be Holder of Bachelor degree or Advanced Diploma in Computer Science,Information Systems,Electrinics or equivalent qualifications
Apply: Secretary, Public
Service Recruitment
Box  63100 ,Dar es Salaam
Details:Daily News April 30, 2012
Deadline:  May   14, 2012

RECORDS MANAGEMENT ASSISTANTS II - 2 POSITIONS
Qualification: Form IV Certificate together with Certificate in records Management from a recognized Institution or equivalent
qualifications
Apply: Secretary, Public
Service Recruitment
Box  63100 ,Dar es Salaam
Details:Daily News April 30, 2012
Deadline:  May   14, 2012

CLINICAL OFFICER  II
Qualification: Ordinary Diploma in Clinical Medicine from a recognized Institution or equivalent
qualifications
Apply: Secretary, Public
Service Recruitment
Box  63100 ,Dar es Salaam
Details:Daily News April 30, 2012
Deadline:  May   14, 2012

LABORATORY TECHNICIAN II
Qualification: Ordinary Diploma in Laboratory Technology from recognized Institution or equivalent
qualifications
Apply: Secretary, Public
Service Recruitment
Box  63100 ,Dar es Salaam
Details:Daily News April 30, 2012
Deadline:  May   14, 2012

COOPERATIVE DEVELOPMENT
Qualification: Masters degree in Coopetarive or equivalent qualifications
Apply: Secretary, Public
Service Recruitment
Box  63100 ,Dar es Salaam
Details:Daily News April 30, 2012
Deadline:  May   14, 2012

YOUTH WORK/GENDER STUDIES
Qualification: Master’s degree in work Gender Studies or equivalent qualifications
Apply: Secretary, Public
Service Recruitment
Box  63100 ,Dar es Salaam
Details:Daily News April 30, 2012
Deadline:  May   14, 2012

LINGUISTICS
Qualification: Master’s degree in Linguistics or equivalent
qualifications
Apply: Secretary, Public
Service Recruitment
Box  63100 ,Dar es Salaam
Details:Daily News April 30, 2012
Deadline:  May   14, 2012

POLITICAL SCIENCE
Qualification: Master’s degree in Political Science or equivalent
 qualifications
Apply: Secretary, Public
Service Recruitment
Box  63100 ,Dar es Salaam
Details:Daily News April 30, 2012
Deadline:  May   14, 2012

BUSINESS ADMINISTRATION /HUMAN RESOURCE MANAGEMENT
Qualification: Master degree in Business Administration, Human Resource Management or
equivalent
Apply: Secretary, Public
Service Recruitment
Box  63100 ,Dar es Salaam
Details:Daily News April 30, 2012
Deadline:  May   14, 2012

ASSISTANT LECTURER - 5 POSITIONS
Qualification:(Bachelor’s Degree)to teach up to NTA level 8
Apply: Secretary, Public
Service Recruitment
Box  63100 ,Dar es Salaam
Details:Daily News April 30, 2012
Deadline:  May   14, 2012

TUTORIAL  ASSISTANT/ASSISTANT LIBRARIAN TRAINEE
Qualification: Bachelor degree in librarianship or equivalent qualification
Apply: Secretary, Public
Service Recruitment
Box  63100 ,Dar es Salaam
Details:Daily News April 30, 2012
Deadline:  May   14, 2012

SOCIAL STUDIES (SOCIOLOGY,POLITICAL SCIENCE AND PUBLIC ADMINISTRATION)
Qualification: Bachelor degree in Sociology,Political Science,Public Administration or equivalent qualification
Apply: Secretary, Public
Service Recruitment
Box  63100 ,Dar es Salaam
Details:Daily News April 30, 2012
Deadline:  May   14, 2012

ACCOUNTANCY
Qualification: Bachelor degree in Accountancy or equivalent qualifications
Apply: Secretary, Public
Service Recruitment
Box  63100 ,Dar es Salaam
Details:Daily News April 30, 2012
Deadline:  May   14, 2012

TUTORIAL  ASSISTANTS - 3 POSTS
Qualification: Bachelor degree in either Computer Science or equivalent qualification
Apply: Secretary, Public
Service Recruitment
Box  63100 ,Dar es Salaam
Details:Daily News April 30, 2012
Deadline:  May   14, 2012

ACCOUNTANT
Qualification: Holder of a degree in Accountancy or Business Administration from a recognized
Institution
Apply: Chief Executive Occupational safety and Health Authority
Box  519 ,Dar es Salaam
Details:Daily News May 03, 2012
Deadline:  May   17, 2012

NURSING OFFICER II - 2 POSITIONS
Qualification: Bachelor degree in Nursing or equivalent qualification from a recognized Institution
Apply: Chief Executive Occupational safety and Health Authority
Box  519 ,Dar es Salaam
Details:Daily News May 03, 2012
Deadline:  May   17, 2012

MEDICAL OFFICER II - 3 POSITIONS
Qualification: Bachelor degree in Medicine or equivalent qualification from a recognized Institution
Apply: Chief Executive Occupational safety and Health Authority
Box  519 ,Dar es Salaam
Details:Daily News May 03, 2012
Deadline:  May   17, 2012

DEPUTY CHIEF EXECUTIVE OFFICER
Qualification: Post Graduate degree in Engineering,(Mechanical Electrical,Civil process,mining or geology),Economics or business Administration
Apply: Managing Director National Development Corporation
Box  2669 ,Dar es Salaam
Details:Daily News May 04, 2012
Deadline:  June   05, 2012

RECEPTIONIST
Qualification: Diploma/Certificate in Secretarial Services/ Office
Management
Apply: The Director of Human Resource Development & Administration Tanzania Post Authority
Box  9184 ,Dar es Salaam
Details:Daily News May 04, 2012
Deadline:  May   18, 2012

DRIVER
Qualification: Secondary School Education,VETA or NIT driving license class C Driving license Apply: The Director of Human Resource Development & Administration Tanzania Post Authority
Box  9184 ,Dar es Salaam
Details:Daily News May 04, 2012
Deadline:  May   18, 2012

EXECUTIVE ASSISTANT
Qualification: Diploma in Secretarial Services/Office Management with typing speed 50 W.P.M & short -hand 100/120 W.P.M in English
Apply: The Director of Human Resource Development & Administration Tanzania Post Authority
Box  9184 ,Dar es Salaam
Details:Daily News May 04, 2012
Deadline:  May   18, 2012

SENIOR QUALITY ASSURANCE OFFICER
Qualification: A University degree in,Statistics or Quality Management
Apply: The Director of Human Resource Development & Administration Tanzania Post Authority
Box  9184 ,Dar es Salaam
Details:Daily News May 04, 2012
Deadline:  May   18, 2012

SENIOR TRAINING OFFICER
Qualification: A University degree in,Business Studies , Information Technology or related field
Apply: The Director of Human Resource Development & Administration Tanzania Post Authority
Box  9184 ,Dar es Salaam
Details:Daily News May 04, 2012
Deadline:  May   18, 2012

HELP DESK OFFICER
Qualification: A Diploma in Mass Communications,Business Management,Information Technology or related field
Apply: The Director of Human Resource Development & Administration Tanzania Post Authority
Box  9184 ,Dar es Salaam
Details:Daily News May 04, 2012
Deadline:  May   18, 2012

INFORMATION TECHNOLOGY TECHNICIAN
Qualification:A Diploma/Advanced Diploma in Computer Engineering, Science Electronic Engineering or equivalent Advanced Diploma
Apply: The Director of Human Resource Development & Administration Tanzania Post Authority
Box  9184 ,Dar es Salaam
Details:Daily News May 04, 2012
Deadline:  May   18, 2012

SENIOR INFORMATION TECHNOLOGY TECHNICIAN
Qualification: A University degree in,Computer Engineering,Electronic Engineering or equivalent advanced Diploma
Apply: The Director of Human Resource Development & Administration Tanzania Post Authority
Box  9184 ,Dar es Salaam
Details:Daily News May 04, 2012
Deadline:  May   18, 2012

SENIOR BUSINESS ANALST - 3 POSTS
Qualification: Bachelor degree in Computer Science,Information Technology,Master degree in Business Management or Administration will be an added advantage
Apply: The Director of Human Resource Development & Administration Tanzania Post Authority
Box  9184 ,Dar es Salaam
Details:Daily News May 04, 2012
Deadline:  May   18, 2012

SENIOR DATABASE ADMINISTRATOR
Qualification: A University degree in Computer Science,Computer Engineering,Electronic Engineering or related fields
Apply: The Director of Human Resource Development & Administration Tanzania Post Authority
Box  9184 ,Dar es Salaam
Details:Daily News May 04, 2012
Deadline:  May   18, 2012

SENIOR SYSTEM ADMINISTRATOR
Qualification: A University degree in Computer Science,Computer Engineering,Electronic Engineering or related fields
Apply: The Director of Human Resource Development & Administration Tanzania Post Authority
Box  9184 ,Dar es Salaam
Details:Daily News May 04, 2012
Deadline:  May   18, 2012

SENIOR NETWORK ADMINISTRATOR
Qualification: A University degree in Computer Science,Computer Engineering,Electronic Engineering or related fields
Apply: The Director of Human Resource Development & Administration Tanzania Post Authority
Box  9184 ,Dar es Salaam
Details:Daily News
May 04, 2012
Deadline:  May   18, 2012

TUTORIAL ASSISTANT/EXAMINATIONS OFFICER
Qualification: Bachelor degree in Educations or equivalent qualifications
Apply: Secretary, Public
Service Recruitment
Box  63100 ,Dar es Salaam
Details:Daily News April 30, 2012
Deadline:  May   14, 2012

ACCOUNTANCY GRADE I 
Qualification: Bachelor degree or Advanced Diploma in Accountancy  or equivalent qualifications
Apply: Secretary, Public
Service Recruitment
Box  63100 ,Dar es Salaam
Details:Daily News April 30, 2012
Deadline:  May   14, 2012

SENIOR INTERNAL AUDITOR 
Qualification: Bachelor degree or Advanced Diploma in Accountancy and CPA (T) or - ACCA or equivalent qualifications
Apply: Secretary, Public
Service Recruitment
Box  63100 ,Dar es Salaam
Details:Daily News April 30, 2012
Deadline:  May   14, 2012

SENIOR ADMINISTRATOR OFFICER
Qualification: Bachelor degree or Advanced Diploma in Public Administration,Sociology, Human Resource Management or
equivalent qualifications
Apply: Secretary, Public
Service Recruitment
Box  63100 ,Dar es Salaam
Details:Daily News April 30, 2012
Deadline:  May   14, 2012

SENIOR SYSTEMS ADMINISTRATOR
Qualification: Must be Holder of Bachelor degree or Advanced Diploma in Computer Science,Information Systems,Electrinics or equivalent qualifications
Apply: Secretary, Public
Service Recruitment
Box  63100 ,Dar es Salaam
Details:Daily News April 30, 2012
Deadline:  May   14, 2012

RECORDS MANAGEMENT ASSISTANTS II - 2 POSITIONS
Qualification: Form IV Certificate together with Certificate in records Management from a recognized Institution or equivalent
Apply: Secretary, Public
Service Recruitment
Box  63100 ,Dar es Salaam
Details:Daily News April 30, 2012
Deadline:  May   14, 2012

CLINICAL OFFICER  II 
Qualification: Ordinary Diploma in Clinical Medicine from a recognized Institution or equivalent
Apply: Secretary, Public
Service Recruitment
Box  63100 ,Dar es Salaam
Details:Daily News April 30, 2012
Deadline:  May   14, 2012

LABORATORY TECHNICIAN II 
Qualification: Ordinary Diploma in Laboratory Technology from recognized Institution or equivalent
qualifications
Apply: Secretary, Public
Service Recruitment
Box  63100 ,Dar es Salaam
Details:Daily News April 30, 2012
Deadline:  May   14, 2012

COOPERATIVE DEVELOPMENT
Qualification: Masters degree in Coopetarive or equivalent qualifications
Apply: Secretary, Public
Service Recruitment
Box  63100 ,Dar es Salaam
Details:Daily News April 30, 2012
Deadline:  May   14, 2012

YOUTH WORK/GENDER STUDIES
Qualification: Master’s degree in work Gender Studies or equivalent qualifications
Apply: Secretary, Public
Service Recruitment
Box  63100 ,Dar es Salaam
Details:Daily News April 30, 2012
Deadline:  May   14, 2012

LINGUISTICS
Qualification: Master’s degree in Linguistics or equivalent
qualifications
Apply: Secretary, Public
Service Recruitment
Box  63100 ,Dar es Salaam
Details:Daily News April 30, 2012
Deadline:  May   14, 2012

POLITICAL SCIENCE
Qualification: Master’s degree in Political Science or equivalent
 qualifications
Apply: Secretary, Public
Service Recruitment
Box  63100 ,Dar es Salaam
Details:Daily News April 30, 2012
Deadline:  May   14, 2012

BUSINESS ADMINISTRATION /HUMAN RESOURCE MANAGEMENT
Qualification: Master degree in Business Administration, Human Resource Management or
equivalent
Apply: Secretary, Public
Service Recruitment
Box  63100 ,Dar es Salaam
Details:Daily News April 30, 2012
Deadline:  May   14, 2012

ASSISTANT LECTURER - 5 POSITIONS
Qualification:(Bachelor’s Degree)to teach up to NTA level 8
Apply: Secretary, Public
Service Recruitment
Box  63100 ,Dar es Salaam
Details:Daily News April 30, 2012
Deadline:  May   14, 2012

TUTORIAL  ASSISTANT/ASSISTANT LIBRARIAN TRAINEE
Qualification: Bachelor degree in librarianship or equivalent qualification
Apply: Secretary, Public
Service Recruitment
Box  63100 ,Dar es Salaam
Details:Daily News
April 30, 2012
Deadline:  May   14, 2012

SOCIAL STUDIES (SOCIOLOGY,POLITICAL SCIENCE AND PUBLIC ADMINISTRATION)
Qualification: Bachelor degree in Sociology,Political Science,Public Administration or equivalent qualification
Apply: Secretary, Public
Service Recruitment
Box  63100 ,Dar es Salaam
Details:Daily News
April 30, 2012
Deadline:  May   14, 2012

ACCOUNTANCY
Qualification: Bachelor degree in Accountancy or equivalent qualifications
Apply: Secretary, Public
Service Recruitment
Box  63100 ,Dar es Salaam
Details:Daily News
April 30, 2012
Deadline:  May   14, 2012

TUTORIAL  ASSISTANTS - 3 POSTS
Qualification: Bachelor degree in either Computer Science or equivalent qualification
Apply: Secretary, Public
Service Recruitment
Box  63100 ,Dar es Salaam
Details:Daily News
April 30, 2012
Deadline:  May   14, 2012.                                                                                                             CHANZO CHA HABARI GAZETI LA MWANANCHI.